Msanii wa hip hop na rapa wa Tanzania Roma Mkatoriki akumbana na adhabu ya kutotoa kazi yoyote ya muziki na kutoshiriki tamasha wala show yoyote kwa muda wa miezi sita kutoka kwenye balaza la wasanii Tanzania BASATA baada ya kutoitikia mwito wa kikao na BASATA. “Huyu ndugu anayeitwa Roma Mkatoliki tunampa adhabu, kwa mujibu wa katiba na kanuni ambazo zinatuongoza sisi. kwa hiyo tunamfungia kwa miezi sita. Ndani ya hiyo miezi sita hakuna kufanya kazi yoyote ya sanaa, hakuna kutoa wimbo wowote wa sanaa, hakuna kuperform kwenye tamasha lolote, na wimbo huo moja kwa moja tunaufungia,” amesema Naibu Waziri, Juliana Shonza. Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi,, Machi 1, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza ameeleza kuwa msanii huyo amewahi kupewa onyo la kubadilisha jina la wimbo huo pamoja na baadhi ya maneno yaliyomo ndani yake, lakini alikaidi na wimbo huo ukaendelea kupigwa katika vyombo mbalimbali vya habari. Shonza ameongez...